Create Yours

Top 120 Enock Maregesi Quotes (2026 Update)
Page 2 of 3

Enock Maregesi Quote: “Maskini mwenye pesa nyingi ni tajiri bahili. Tajiri mwenye mifuko iliyotoboka ni tajiri badhiri.”
Enock Maregesi Quote: “Wakati mwingine unakokwenda siko. Rudi nyuma. Ukirudi nyuma huko nyuma ndiko mbele yako.”
Enock Maregesi Quote: “Lengo kuu la Shetani kuingilia uumbaji wa Mungu kwa kutumia Succubus na Incubus ni kumzuia Yesu asirudi kwa mara ya pili. Anajua akiingilia uumbaji huo na kuwafanya watu wote wawe na roho za kishetani, wokovu hautakuwa na maana, Yesu hatakuwa na mtu wa kumwokoa atakaporudi kwa mara ya pili.”
Enock Maregesi Quote: “Kinachotokea katika dunia hii si kitu kizuri cha kuzoea au hata kufikiria. Hivyo tuna haki ya kuwa na mawazo, hasira na wanyonge kuhusiana na suala zima la maisha yetu hapa duniani. Hata hivyo hali hii itabaki kuwa hivyo kwa sababu Mungu ametaka iwe hivyo kwa sasa. Kwa maana hiyo, hekima ni kukubaliana na mapenzi ya Mungu. Lazima tukubaliane na kisichoweza kufikirika kuweza kubadilika.”
Enock Maregesi Quote: “Amani ya nafsi ni zaidi ya amani ya kisiasa. Amani ya kisiasa itaweza kupatikana endapo watu watakuwa na amani ndani ya mioyo yao. Watu wakiithamini amani na kuielewa watayafurahia maisha yao, na mataifa yakiithamini amani na kuielewa yatastawi. Vita hutengenezwa ndani ya mioyo ya watu. Ukiitafuta amani ndani ya moyo wako, taifa halitasimama kupigana na taifa, amani itaweza kupatikana.”
Enock Maregesi Quote: “Jina la Yesu ni kubwa kuliko majina yote duniani na hata kuzimu. Lazima Shetani aliogope kuliko anavyomwogopa Bikira Maria au sakramenti za aina zote. Kumbuka, jina la Yesu halitajwi kilingeni. Linatajwa kanisani, ambapo linatajwa kinafiki. Hivyo, aliye na mamlaka ya kuaminiwa na kuabudiwa na aponyaye ni Yesu Kristo peke yake.”
Enock Maregesi Quote: “Pesa ina maana kwa sababu ya wanawake.”
Enock Maregesi Quote: “Wajerumani, hata hivyo, wakati wa utawala wao waliruhusu Kiswahili kiwe lugha halisi ya taifa nchini Tanzania kwa vile hawakukiongea Kiingereza wala hawakukipenda. Ndiyo maana Kiswahili kinazungumzwa zaidi nchini Tanzania kuliko Kenya au Uganda.”
Enock Maregesi Quote: “Ukipata matatizo kumbuka kwamba Yesu alipata matatizo pia, na kutokana na matatizo hayo mimi na wewe tulipata uhuru. Soma Biblia. Soma nyimbo katika kitabu cha Zaburi zinazomsifu Mungu katika kipindi cha matatizo. Funga na kuomba ukiamini kwamba mapenzi ya Mungu kwetu ni huru, yasiyokuwa na masharti yoyote. Toa msamaha kwa waliokukosea. Ni kitu cha muhimu kujilimbikizia imani katika kipindi cha amani, ili matatizo yakitokea usiweze kuyumba.”
Enock Maregesi Quote: “Ubatizo ni toba iletayo ondoleo la dhambi. Mwangushe Goliati wa uzinzi katika maisha yako kwa kumtumia Yesu Kristo, ambaye ni Daudi wa mapandikizi yote ya dhambi katika maisha yetu.”
Enock Maregesi Quote: “Ukitaka watu wakuheshimu usitumie mabavu. Tumia hekima. Maana, watu hawaheshimu wewe ni nani au unatoka wapi, wanaheshimu nguvu ya matendo yako. Kama una tatizo na mtu usichukue uamuzi wa haraka. Ongea na watu kupata hekima.”
Enock Maregesi Quote: “Maisha yangu ni darasa. Jifunzeni kutokana na maisha yangu, jifunzeni kutokana na sifa zangu za ushupavu, jifunzeni kutokana na sifa zangu za udhaifu, kutatua matatizo katika maisha yenu.”
Enock Maregesi Quote: “Yesu wakati anakufa msalabani hakufikiria kifo. Alifikiria maisha.”
Enock Maregesi Quote: “Katika jiji la Dar watu hawaendi kazini. Wanakwenda vitani. Wania kilicho chako ukidhulumiwa. Utajiri humpendelea anayejaribu.”
Enock Maregesi Quote: “Utajiri wa nje huwa unaanzia ndani, nao ni hekima.”
Enock Maregesi Quote: “Ukiwa mchapakazi hodari mwenye msimamo na nia thabiti ya utendaji kazi unaweza kuwa mpweke kwa maana ya kuwa na marafiki wachache. Lakini mashabiki utakuwa nao wengi.”
Enock Maregesi Quote: “Robert Louis Stevenson wa Uskochi aliponukuu nahau ya ‘kamera haiwezi kudanganya’ katika kitabu chake cha ‘South Seas’ mwaka 1896, miaka 57 baada ya sanaa ya upigaji wa picha kugunduliwa, hakumaanisha tuwe asili. Hakumaanisha tusizirekebishe picha zetu baada ya kuzipiga na kuzisafisha! Alimaanisha tuwe nadhifu tuonekanapo mbele za watu au mbele ya vyombo vya habari; ambapo picha itapigwa, itasafishwa, itachapishwa na itauzwa kama ilivyo bila kurekebishwa.”
Enock Maregesi Quote: “Kiswahili ni lugha rasmi ya nchi za Tanzania, Kenya na Uganda. Ni lugha isiyo rasmi ya nchi za Rwanda, Burundi, Msumbiji na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Lugha ya Kiswahili ni mali ya nchi za Afrika ya Mashariki, si mali ya nchi za Afrika Mashariki peke yake. Pia, Kiswahili ni lugha rasmi ya Umoja wa Afrika; pamoja na Kiarabu, Kiingereza, Kifaransa, Kireno na Kihispania. Kiswahili ni lugha inayozungumzwa zaidi nchini Tanzania kuliko nchi nyingine yoyote ile, duniani.”
Enock Maregesi Quote: “Kuzaliwa na kuishi ni mibaraka mikubwa ya Mwenyezi Mungu kuliko yote duniani.”
Enock Maregesi Quote: “Wape watoto wako urithi wa kutosha ili waweze kufanya kitu, lakini si urithi wa kutosha ili wasiweze kufanya kitu. Wape watoto uhuru wanaostahili kupata, uhuru wa mahesabu, lakini si uhuru wa kila kitu.”
Enock Maregesi Quote: “Watu wakikuonyesha tabia zao za ndani kabisa waamini. Wanajijua vizuri zaidi, kuliko unavyowajua.”
Enock Maregesi Quote: “Kama John Doe ana matatizo katika maisha yake acha ayatatue mwenyewe. Akishindwa atakuomba ushauri au ataomba ushauri kutoka kanisani kama ni Mkristo, au msikitini kama Mwislamu, au kutoka katika nyumba yoyote ya ibada kulingana na imani yake. Mtu akikuomba ushauri mshauri kwa moyo wako wote, wala usimshauri kwa unafiki au kinyongo cha aina yoyote ile.”
Enock Maregesi Quote: “Wakati ndege inapaa huwa inapambana na upepo. Lakini inapaa, hata hivyo.”
Enock Maregesi Quote: “Luka 22:20 ni mwisho wa agano la kale la damu za wanyama na mwanzo wa agano jipya la damu ya Yesu.”
Enock Maregesi Quote: “Mungu alilibariki taifa la Israeli katika misingi ya kidini na si katika misingi ya kisiasa au misingi ya kihistoria; na asili ya dini ya Kikristo ni kutoka katika taifa hilo ambalo Biblia imelitaja kama taifa teule la Mwenyezi Mungu. Mgogoro wa Israeli na Palestina ulianzishwa na Israeli mwenyewe. Yakobo alipokea baraka iliyokuwa si ya kwake kwa kutumia hila ya Rebeka. Baraka ya Yakobo ilikuwa ya Esau.”
Enock Maregesi Quote: “Kila kipato kina mashetani yake, mengine mazuri na mengine mabaya, lakini mengi ni mabaya. Wakati mwingine maskini ahitaji pesa, pesa anaweza kushindwa kuidhibiti, anahitaji paa na kuta nne kujisetiri yeye na familia yake.”
Enock Maregesi Quote: “Mojawapo ya misingi ya ujasusi ni kuwa na uwezo wa kutofautisha kati ya unachojua, usichojua na unachofikiria. Unaweza kusema unajua wakati hujui. Maamuzi yasiyo sahihi ya kijasusi huweza kuiletea tume madhara makubwa.”
Enock Maregesi Quote: “Ukitaka kufanikiwa katika maisha angalia watu wanataka nini halafu wape. Kama wanataka burudani wape. Kama wanataka elimu wape. Kama wanataka bidhaa wape. Kama wanataka huduma wape. Wape kwa msaada wa wataalamu.”
Enock Maregesi Quote: “Nuhu anasemekana kuwa mtu aliyedharaulika sana huko Babeli. Maisha yake yalijaa utata. Lakini ukweli ni kwamba, bila Nuhu mimi na wewe tusingekuwapo. Unayemdharau sana mwogope sana.”
Enock Maregesi Quote: “Words are the bricks of our world and they have the power to change it.”
Enock Maregesi Quote: “Success is a test.”
Enock Maregesi Quote: “Kipimo cha hofu ya Mungu ni kumjua!”
Enock Maregesi Quote: “Kila mtu anapaswa kuwa na siri angalau moja katika maisha yake.”
Enock Maregesi Quote: “Kitabu cha ‘Kolonia Santita’ ni kitabu cha wasomi na wasiokuwa wasomi, watu wa mijini na watu wa vijijini, watu wazima, vijana na watoto. Hadhira ya kitabu hiki ni jamii nzima ya Tanzania.”
Enock Maregesi Quote: “Kama utafiti wa mtu umevuka mipaka ya ukweli au uhalisia toa utafiti mwingine kuupinga huo wa kwake, kwa lengo la kuelimisha wengi. Haina maana kusema jambo si la kweli na usitwambie kwa nini si la kweli.”
Enock Maregesi Quote: “Wazazi wetu ni watu wa kuheshimu kuliko kitu kingine chochote kile kwa sababu wana uwezo wa kuona tusipoweza kuona. Yaani, wanajua kilichokuwepo kabla ya sisi kuzaliwa na wanajua kilichokuwepo baada ya sisi kuzaliwa. Maisha tuliyopitia, wazazi wetu walishapitia. Tulipokuwa, wazazi wetu walishakuwepo; na tulichofanya, wazazi wetu walishafanya. Hivyo, hatuna budi kuwaheshimu wazazi wetu. Lakini, wazazi wetu wanapaswa kujiheshimu kutufundisha adabu na maadili mema.”
Enock Maregesi Quote: “Heri kuwa Mkristo wa Yesu Kristo, au Mwislamu wa Mtume Muhammad, kuliko kuwa mkristo wa kanisa au mwislamu wa msikiti.”
Enock Maregesi Quote: “Ukiona kitu ambacho hukupaswa kuona, au ukisikia kitu ambacho hukupaswa kusikia, fumba macho kwa kuyakodoa! Ulichokiona au kukisikia usikiseme leo na hata milele. Jifanye hukuona kitu, hukusikia kitu. Ukifumbua macho kwa kuyakodoa utapata matatizo, makubwa.”
Enock Maregesi Quote: “Mungu akikubariki kipaji chako watu watasema ni laana. Maisha yako ni sawa na mto. Unakoelekea ni baharini. Lakini sasa umefika kwenye mlango wa bahari. Unahangaika upite wapi kufika baharini, ambapo utaogelea kwa kadiri utakavyoweza. Utakapofika baharini, watu, badala ya kusema umebarikiwa, watasema umelaaniwa, badala ya kukuita malaika, watakuita shetani. Mafanikio hayapimwi kwa pesa au mali kiasi gani unayo, mafanikio yanapimwa kwa amani ya moyo au maisha ya watu kiasi gani umeboresha.”
Enock Maregesi Quote: “Ujasusi ni kitu cha muhimu kwa maendeleo ya nchi yoyote. Watu wanaoshughulika na ujasusi wanapaswa kuwa makini mno kwani kazi yao ni nyeti sana kulinganisha na kazi za watu wengine. Kosa dogo la kiusalama linaweza kubadili mwelekeo wa historia ya nchi.”
Enock Maregesi Quote: “Kukiuka Amri Kumi za Mungu si dhambi ni matawi ya dhambi. Dhambi ni kumkana Mungu na kumkubali Shetani.”
Enock Maregesi Quote: “Chukia kushindwa, zaidi ya unavyofurahia kushinda.”
Enock Maregesi Quote: “Acha alama katika dunia baada ya kuondoka.”
Enock Maregesi Quote: “There are many internal secrets that make a person continue to succeed, and there are many external secrets that make a person continue to hide their secrets. Internal secrets are true secrets, while the outer secrets are false secrets, aimed at hiding the truth. However, the secret to success is hard work, knowledge and secrecy.”
Enock Maregesi Quote: “We are the children of Nelson Mandela; we are the children of Kwame Nkrumah; we are the children of Haile Selassie; we are the children of Samora Machel; we are the children of Robert Mugabe; we are the children of Patrice Lumumba; we are the children of Julius Kambarage Nyerere. We know who we are.”
Enock Maregesi Quote: “Mbili jumulisha mbili wakati mwingine si sawa na nne. Ni sawa na nne jumulisha moja kwa sababu moja ni nguvu ya ushirikiano.”
Enock Maregesi Quote: “If a leader for the right reasons is blessed by God, even the people he leads will be blessed by God as well. But if the leader is cursed by God because of iniquity, even the people he leads will be cursed as well.”
Enock Maregesi Quote: “Mungu alisema tupendane katika shida na raha; Luka 6:27-36. Katika matatizo mpende hasimuyo. Maumivu ya watu hufanana.”
Enock Maregesi Quote: “Kushirikiana na maadui wa nchi yetu ni hatia ya kosa la uhaini. Adhabu yake ni kifo, au kifungo cha maisha.”
Enock Maregesi Quote: “Mpenzi. Sikiliza. Magaidi yaliyomuua Marciano yana mtandao dunia nzima na watu wote wanayajua. Yanaitwa Kolonia Santita. Tatizo hata hivyo ni moja: Hakuna mtu amewahi kuthibitisha au kutoa ushuhuda wa uhalifu wao ili watiwe nguvuni. Huendesha maisha yao kibabe na yana kila mbinu ya kukwepa sheria, ndani na nje ya Meksiko. Watu wengi wameuwawa kwa sababu ya Kolonia Santita. Ukileta kidomodomo yanakuua; au yanakupa notisi ya kuhama mji au nchi, ukakae mbali na Meksiko au Mexico City.”
PREV 1 2 3 NEXT
Motivational Quotes
Inspirational Entrepreneurship Quotes
Positive Quotes
Albert Einstein Quotes
Startup Quotes
Steve Jobs Quotes
Success Quotes
Inspirational Quotes
Courage Quotes
Life Quotes
Focus Quotes
Swami Vivekananda Quotes

Beautiful Wallpapers and Images

We hope you enjoyed our collection of 120 Enock Maregesi Quotes.

All the images on this page were created with QuoteFancy Studio.

Use QuoteFancy Studio to create high-quality images for your desktop backgrounds, blog posts, presentations, social media, videos, posters, and more.

Learn more