Top 100

Top 120 Enock Maregesi Quotes (2024 Update)
Page 3 of 3

Enock Maregesi Quote: “Yesu wakati anakufa msalabani hakufikiria kifo. Alifikiria maisha.”
Enock Maregesi Quote: “Kukiuka Amri Kumi za Mungu si dhambi ni matawi ya dhambi. Dhambi ni kumkana Mungu na kumkubali Shetani.”
Enock Maregesi Quote: “Chukia kushindwa, zaidi ya unavyofurahia kushinda.”
Enock Maregesi Quote: “Lakini Kiswahili kilizaliwa Afrika Mashariki. Kwa nini hatuithamini lugha yetu? Kwa nini hatuzithamini lugha zetu za makabila? Kwa nini hatuipendi na kuitetea lugha yetu ya taifa ambayo ndiyo lugha ya biashara na mawasiliano ya Afrika Mashariki? Kwa nini hatuvitetei vizazi vijavyo kwa kuvitetea vizazi vya leo?”
Enock Maregesi Quote: “Watu wa kulisaidia bara la Afrika hawatatoka Amerika au kwingineko. Afrika ni tatizo letu. Watatoka Afrika kwenyewe.”
Enock Maregesi Quote: “Kuwa makini na kila kitu unachofanya kwa maana ubongo ni kitu cha ajabu, ubongo una uwezo wa kukupotosha.”
Enock Maregesi Quote: “Wajerumani, hata hivyo, wakati wa utawala wao waliruhusu Kiswahili kiwe lugha halisi ya taifa nchini Tanzania kwa vile hawakukiongea Kiingereza wala hawakukipenda. Ndiyo maana Kiswahili kinazungumzwa zaidi nchini Tanzania kuliko Kenya au Uganda.”
Enock Maregesi Quote: “Mungu anaweza kusamehe kutokujua kwetu kwa sababu hatuwezi kukiamini kile tusichokijua; na hata kama tutaweza kuadhibiwa kwa kile tusichokijua, hatutaweza kuadhibiwa vikali kama ambavyo tutaweza kuadhibiwa kwa kile tunachokijua.”
Enock Maregesi Quote: “Bila Masihi hakuna atakayetunukiwa tiketi ya kuingia katika ufalme wa Mungu, kwa sababu hakuna atakayeokolewa bila Masihi.”
Enock Maregesi Quote: “Watanzania wengi hawana mzuka na kazi, ndiyo maana wanashindwa.”
Enock Maregesi Quote: “Kama una akili kuwa kawaida. Kama una nguvu kuwa mkarimu. Kama una pesa kuwa mnyenyekevu. Ukitaka kuwa na akili kuwa kawaida. Ukitaka kuwa na nguvu kuwa mkarimu. Ukitaka kuwa na pesa kuwa mnyenyekevu.”
Enock Maregesi Quote: “Without true opposition the country can not be ruled, although it can be dominated without true opposition. To be ruled is to accept to be dominated; to be dominated is to accept to be ruled. Without true opposition there is no true patriotism; without true patriotism there is no true opposition. Be a true opponent of the government, by being a true patriarch of your country; defend your country from the heart, on the fundamental issues of the country’s constitution.”
Enock Maregesi Quote: “Toa msamaha kwa waliokukosea kwa sababu dhambi zilizofanya mkosane zilitoka kwa Shetani.”
Enock Maregesi Quote: “Lolote unalolifikiria yupo mtu mahali fulani duniani ameshalifikiria.”
Enock Maregesi Quote: “Ukiua mtu bila kumwambia kwa nini unamuua anaweza kujua umemuua kwa kumwonea. Akijua umemuua kwa kumwonea roho yake inaweza kukusumbua wewe na familia yako maisha yenu yote. Makachero wa EAC wana leseni ya kuua. Lakini si kuua ovyo kama James Bond. Kila wanayemuua lazima waandike ripoti kwa nini wamemuua. Kachero wa EAC akiua mtu, kwa makosa, kwa bahati mbaya, atalindwa na Mwenyezi Mungu. Atalindwa na Tambiko la Tume ya Dunia.”
Enock Maregesi Quote: “Ukitaka watu wakuheshimu usitumie mabavu. Tumia hekima. Maana, watu hawaheshimu wewe ni nani au unatoka wapi, wanaheshimu nguvu ya matendo yako. Kama una tatizo na mtu usichukue uamuzi wa haraka. Ongea na watu kupata hekima.”
Enock Maregesi Quote: “Ramachandra maana yake ni mwezi. Mwezi ni setilaiti na mwezi unamulika. Ramachandra anaitwa setilaiti kwa sababu ya umuhimu wake katika bara la Asia. Anamulika India na bara zima la Asia, na Australia, kwa niaba ya Kolonia Santita. Ana miaka 44. Ana mke na watoto 6. Ni jambazi aliyekubuhu wa India.”
Enock Maregesi Quote: “Ukiwa mchapakazi hodari mwenye msimamo na nia thabiti ya utendaji kazi unaweza kuwa mpweke kwa maana ya kuwa na marafiki wachache. Lakini mashabiki utakuwa nao wengi.”
Enock Maregesi Quote: “Mwili wako una uwezo wa kujua kabla yako kitakachotokea baadaye. Kama una njaa kwa mfano, mwili wako utakwambia. Kama una kiu, mwili wako utakwambia. Kama unaumwa, mwili wako utakwambia. Kama kuna kitu kibaya kinatarajia kutokea katika maisha yako au katika maisha ya mtu mwingine, mwili wako utakwambia. Kuwa makini na alamu zinazotoka ndani ya mwili wako, kwani hizo ni ishara za Roho Mtakatifu kukuepusha na matatizo ya dunia hii.”
Enock Maregesi Quote: “Kadiri unavyozidi kupanda juu ndivyo utakavyoanguka vibaya.”
Enock Maregesi Quote: “Mungu akikubariki kipaji chako watu watasema ni laana. Maisha yako ni sawa na mto. Unakoelekea ni baharini. Lakini sasa umefika kwenye mlango wa bahari. Unahangaika upite wapi kufika baharini, ambapo utaogelea kwa kadiri utakavyoweza. Utakapofika baharini, watu, badala ya kusema umebarikiwa, watasema umelaaniwa, badala ya kukuita malaika, watakuita shetani. Mafanikio hayapimwi kwa pesa au mali kiasi gani unayo, mafanikio yanapimwa kwa amani ya moyo au maisha ya watu kiasi gani umeboresha.”
Enock Maregesi Quote: “Baraka inapotoka kwa Mungu lengo lake ni kukufanya umpende Mungu kupitia wenzako.”
Enock Maregesi Quote: “Lengo kuu la Shetani kuingilia uumbaji wa Mungu kwa kutumia Succubus na Incubus ni kumzuia Yesu asirudi kwa mara ya pili. Anajua akiingilia uumbaji huo na kuwafanya watu wote wawe na roho za kishetani, wokovu hautakuwa na maana, Yesu hatakuwa na mtu wa kumwokoa atakaporudi kwa mara ya pili.”
Enock Maregesi Quote: “Hasanati ni matendo mema. Mema yanatoka kwa Mungu. Mabaya yanatoka kwa Shetani. Mke mwema anatoka kwa Mungu. Mke mbaya anatoka kwa Shetani. Mke mwema ana hekima na busara, ana maadili na tabia njema, ana utu na uchapakazi, ana wema na upendo, na ana aibu kwa wanaume.”
Enock Maregesi Quote: “Kuna maisha baada ya saa tisa na nusu. Kuwa makini na raia.”
Enock Maregesi Quote: “Mungu hagawi pesa kwa watu kama watu wanavyofikiria. Anagawa upendo na hekima.”
Enock Maregesi Quote: “Mungu alikupa maisha akakupa akili ili utambue jema na baya na akakupa amri zake ili uishi kwa amani na upendo. Kama Mungu hayupo mwanamume na mwanamke walitoka wapi? Wazazi wako walitoka wapi? Wazazi wao walitoka wapi? Wazazi wao walitoka wapi?”
Enock Maregesi Quote: “Ukiua mtu damu yake itakusuta maisha yako yote! Itaongea na wewe ikikulaumu milele!”
Enock Maregesi Quote: “Mahatma Gandhi alipigwa risasi na kufariki dunia baada ya maisha yake kumfelisha. Lakini kifo chake kiliipatia India uhuru kutoka Uingereza. Hivyo, akafanikiwa.”
Enock Maregesi Quote: “Kupata maarifa kutokana na shida ni jambo la kawaida, lakini kupata maarifa bila shida ni hekima.”
Enock Maregesi Quote: “Jina la Yesu ni kubwa kuliko majina yote duniani na hata kuzimu. Lazima Shetani aliogope kuliko anavyomwogopa Bikira Maria au sakramenti za aina zote. Kumbuka, jina la Yesu halitajwi kilingeni. Linatajwa kanisani, ambapo linatajwa kinafiki. Hivyo, aliye na mamlaka ya kuaminiwa na kuabudiwa na aponyaye ni Yesu Kristo peke yake.”
Enock Maregesi Quote: “People think that other international languages are smarter and more business wise. But they have to understand that we have to preserve our culture.”
Enock Maregesi Quote: “Kitu cha kwanza kufanya kama umeamua kuficha ukweli wape watu ukweli mwingine kulinda thamani ya utu wako.”
Enock Maregesi Quote: “Wakati ndege inapaa huwa inapambana na upepo. Lakini inapaa, hata hivyo.”
Enock Maregesi Quote: “Kama utafiti wa mtu umevuka mipaka ya ukweli au uhalisia toa utafiti mwingine kuupinga huo wa kwake, kwa lengo la kuelimisha wengi. Haina maana kusema jambo si la kweli na usitwambie kwa nini si la kweli.”
Enock Maregesi Quote: “Write as much as you can. Read as much as you can. Use the library and the internet carefully for research and talk to people about things that matter. If you have an idea in your head talk it to people as a normal conversation, to get their natural opinions. And don’t forget to jot down discreetly any new ideas you get from people. God may use other people to convey messages to you, that may add more information to the ideas you already have.”
Enock Maregesi Quote: “Ujasusi ni kitu cha muhimu kwa maendeleo ya nchi yoyote. Watu wanaoshughulika na ujasusi wanapaswa kuwa makini mno kwani kazi yao ni nyeti sana kulinganisha na kazi za watu wengine. Kosa dogo la kiusalama linaweza kubadili mwelekeo wa historia ya nchi.”
Enock Maregesi Quote: “Usisubiri Mungu afanye kitu ambacho Mungu anasubiri ufanye.”
PREV 1 2 3 NEXT
Motivational Quotes
Inspirational Entrepreneurship Quotes
Positive Quotes
Albert Einstein Quotes
Startup Quotes
Steve Jobs Quotes
Success Quotes
Inspirational Quotes
Courage Quotes
Life Quotes
Swami Vivekananda Quotes
Focus Quotes

Beautiful Wallpapers and Images

We hope you enjoyed our collection of 120 free pictures with Enock Maregesi Quotes.

All of the images on this page were created with QuoteFancy Studio.

Use QuoteFancy Studio to create high-quality images for your desktop backgrounds, blog posts, presentations, social media, videos, posters and more.

Learn more